MHE. MCHENGERWA AIPONGEZA DSTV KWA KUTANGAZA MAUDHUI YA KITANZANIA

 


*************************

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa Kongole kwa Kampuni ya Multichoice Tanzania (DSTV) kwa kurusha maudhui ya kitanzania hususan Muziki na Filamu ambayo yameleta manufaa kwa wasanii.

Mhe. Mchengerwa ametoa pongezi hizo leo Februari 3, 2022 wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Jacqueline Woiso katika ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma.

"Nitakutana na wasanii wote wakiwemo waigizaji na wanamuziki na kufanya nao mazungumzo, hii itatuwezesha kujua changamoto zao na mahitaji yao katika kufanya kazi zao za sanaa na hili ningeomba ushirikiano kutoka kwenu Multichoice Tanzania ili kuweza kufanikisha,"amesema Mhe. Mchengerwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi huyo, ameahidi ushirikiano wa karibu na Wizara katika kuhakikisha sanaa inakuwa na wasanii wanapata kipato kutokana na kazi zao.

Comments

Popular posts from this blog

Mhe. Mhengerwa -Tamasha la Sanaa Bagamoyo ni la kimataifa, Makamu wa Rais afafanua kuwa Sanaa inaongoza katika ukuaji wa uchumi nchini

MOROCCO YAKUBALI KUSHIRIKIANA NA TANZANIA KWENYE MICHEZO

Diamond apongeza Serikali ya Rais Samia kwa kuwasaidia wasanii, kurejesha tuzo